Skip to Content

MATANGAZO DOMINIKA PILI YA MWAKA A

18 Januari 2026 na
MATANGAZO DOMINIKA PILI YA MWAKA A
St Peter's Catholic Church, Administrator
| Hakuna maoni bado

Matangazo ya Parokia

  1. Tunawashukuru sana jumuiya ya Mt. Martin wa Pores waliosafisha Kanisa jana. Idadi yao ni 12. Wiki ijayo ni zamu ya Jumuiya ya Mt. Polycarp wakifuatiwa naJumuiya ya Mt. Hyasinta.

  2. Mafundisho ya Komunio ya Kwanza na Kipaimara kwa lugha ya Kiingereza yataanza Jumamosi ijayo tarehe 24/01/2026. Siku za mafundisho ni kila Jumamosi na Jumapili. Saa 02:00 asubuhi Mpaka 04:00.

  3. Baba Paroko atakuwa na kikao na Wenyeviti na Watunza Fedha wa Kanda zote 8 Dominika ya tarehe 25/01/2026 mara baada ya Misa ya pili Kwenye darasa la Mikutano. Wahusika wote wanaombwa kuhudhuria wito huo wa Baba Paroko bila kukosa. Aidha, kila Kanda itawasilisha kwake siku hiyo ratiba ya Misa za Kanda kwa mwaka mzima wa 2026.

  4. Baba Paroko ameanza tena ziara za Kichungaji za kubariki nyumba za Wana Parokia ambazo hazikuwa zimefikiwa. Kwa wahusika tunaombwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa viongozi wa jumuiya na Kanda ili Paroko aweze kuhitimisha zoezi hili kwa awamu hii.

  5. Kwaya ya Moyo Mt wa Yesu ya hapa Parokiani, watazindua album ya nyimbo katika picha mjongeo(video) siku ya tar. 15/02/2026 kuanzia saa kumi kamili jioni.

    Tiketi zinapatikana nje ya kanisa kwa bei zifuatazo:

    • TZS30,000

    • TZS50,000

    • TZS100,000(VIP)

    • Meza ya VIP kwawatu 10kwaTZS 1,000,000

    Karibuni tuwaunge mkono katika uinjilishaji.

  6. MATANGAZO YA NDOA

    TANGAZO LA KWANZA

    • Charles Beatus Mbunda na Bertina Daniel Mpachoka

    • Wilfred Ambokile Mapunda na Helena Agnel Nalinga

    • Gabriel Edward Mliga na Carolina Gerald Nyasingo

    • Gilbert Abel Munishi na Anastazia Ambrose Njau

    • Jackson Lucas Hugo na Joyce Ali

    • Deokary Dia Msigwa na Adorofina William

MATANGAZO DOMINIKA PILI YA MWAKA A
St Peter's Catholic Church, Administrator 18 Januari 2026
Shiriki posti hii
Sign in to leave a comment